Monday, January 26, 2009

SANAA YA UCHONGAJI YA MAKONDE
Watu wa Makonde walirithi kwa kuishi juu ya uwanda mrefu na wametoka Tanzania ya kusini au Mozambique ya kaskazini. Wameepa ukoloni kwa muda mrefu na watu wenye nguvu na wakali, mara nyingine wameitwa Mawia. Sanaa ya uchongaji imewasaidia watu wa Makonde wamechuma. Wachongaji wengi hutumia mbao laini kama mpingo. Wanachonga vitu kama kiuchumi vyupa vya kizibo, vyombo vya dawa, mitemba, mafimbo, na kadhalika.


Sanaa ya Makonde ina mitindo miwili mikuu, mitindo hii ni Binadamu na Shetani. Mtindo wa Binadamu unaonyesha umbo la asilia na watu katika sanaa hufanya kazi ya kila siku. Mtindo wa Shetani unaonyesha umbo la roho au dini. Watu wa Makonde wanaamini kwamba mchongaji alimwumba Mmakonde wa kwanza. Hadithi ni...

"Katika mwanzo, kiumbe kilitembea duniani, kiumbe hiki hakikuwa mtu au mnyama. Mara nyingine, kiumbe kilikuwa mpweke na siku moja kilipata mbao kutoka mti na kilichonga umbo. Siku ya pili umbo hili lilikuwa na uhai na likakuwa mke wa kiumbe. Mke alizaa mtoto lakini katika siku tatu mtoto akafa. Mke aliona mauti kama kitu kibaya. Kiumbe na mke walihama kutoka mto. Tena, mke alizaa mtoto mwingine na siku ya tatu mtoto akafaa tena. Walihama tena kawa uwanda mrefu. Mke alizaa mtoto wa tatu lakini muda huu mtoto aliishi na mtoto huyu alikuwa Mmakonde wa kwanza au mtu wa kwanza."


Watu wa Makonde wanaamini kuchonga ni muhimu sana kwa sababu kabla ya mtu, kulikuwa mchongaji. Sanaa ya kwanza ilionyesha umuhimu wa wanawake. Iliwakumbusha kwamba mama ndiye aliwapa uhai. Picha ya mama ilichongwa kutoka mbao ilikuwa umbo la ulinzi. Watu walileta uchongaji huu kwa safari. Leo, sanaa ya Makonde ni tofauti. Sanaa nyingine ina dhahania na inaonyesha Mungu, roho na shetani. Wasanii wa Makonde wanatumia mawazo katika uchongaji wao kama nasaba baina ya uhai na mauti au shindano baina ya uzuri na ubaya. Uchongaji si utuli na sanaa ina mwendo au inaamba hadithi.



Habari Zaidi
(Online Exhibit) http://www.makonde-museum.de/
(Article) http://findarticles.com/p/articles/mi_m0438/is_3_35/ai_98171012
http://www.caacart.com/country.php?id=10

Thursday, January 15, 2009

SANAA YA TINGA TINGA
Sanaa ya Tinga Tinga iko aina ya sanaa ya Afrika ya Mashariki. Inatoka nchi za Tanzania na Zanzibar. Sanaa chache inapelekwa nchini ya Kenya kwa sababu inapendwa na watalii. Watalii ambao hutoka nchi za Norway, Sweden, Finland, Denmark, Switzerland na Japan hasa wanapenda sanaa ya Tinga Tinga.


Eduardo Saidi Tingatinga yako mwumbaji wa sanaa ya Tinga Tinga. Tingatinga alizaliwa nchini ya Mozambique lakini alienda mjini wa Dar es Salaam katika mwaka wa elfu moja mia tisa hamsini na tano. Katika mwaka wa elfu moja mia tisa sitini na tano Eduardo Saidi alianza kuzipiga picha. Tingatina alifahamu aliweza kuchuma na picha zake. Wasanii wengi hupiga picha kuchuma na hawapigi picha kwa wenyewe. Katika mwaka wa elfu moja mia tisa sabini na mbili, Eduardo Tingatinga alipigwa bunduki na polisi. Baada ya alifa, rafiki wake walianza ushirika wa chama cha Tingatinga. Chama cha ushirika hiki kiliendelea kuwa shule ya sanaa ya Tingatinga kwa wansanii wa Zanzibar, Dar es Salaam, na kadhalika. Ushirika wa Chama cha ushirika ya Sanaa ya Tinga Tinga una wanachama hamsini na makao makuu karibu na stesheni ya Morogoro katika Dar es Salaam.


Wasanii wanaendeleza kupiga Sanaa ya Tinga Tinga. Sanaa hii inatumia rangi ya baisikeli kwa mazonite zaidi. Picha ya zamani ina mahali ya nyuma wazi na inakuwa pamoja na wanyama kama simba, twiga, kifaru, ndege, na kadhalika. Sanaa ya Tinga Tinga nyingine kuhusu methali na hadithi za kale. Eduardo Tingatinga alitumia methali ya kabila ya Makua. Sanaa hii ni sanaa ya mji lakini ina picha za vijijini.

Wasanii wengine ambao hupiga picha ya sanaa ya Tingatinga ni Simon George Mpata, Jaffari Aussi, na Mikidadi Bush Bohary. Georges Lilanga Di Nyama au George Lilanga hupiga picha pia katika mtindo wa Tingatinga. Mimi ninapenda sana sanaa yake. Lilanga alizaliwa mwaka wa elfumoja mia tisa arobaini na nne. Lilanga ni Makonde na mwanzoni alijifunza kuyachonga mashina ya Kassava. Baadaye, alihama mjini wa Dar es Salaam. George alianza chama cha ushirika kinaitcho Nyumba ya Sanaa. Alijifunza zaidi kuhusu kuchonga na kuchora. Sanaa yake inaungana utamaduni ya Makonde kama shetani na ujamaa.

Watoto Wangu Wanasema Hii Siyo Bei Kubwa